Hitimisho la Semina ya Jinsi ya Kushinda Majaribu Kiroho/Kimwili.
Shaloom
wana wa Mungu,napenda kushukuru Mungu kwa wakati huu ambayo tunaenda
kuhitimisha semina yetu ambayo kiukweli kama ulishiriki vyema toka mwanzo
tulipoanza siku ya Jumatatu tarehe 7th September 2015,basi nina
imani kwamba semina hii itakuwa imekutoa hatua moja kwenda nyingine kiroho.Wale
walio bahatika kuhudumu wametumia mioyo yao vyema, wakatumiwa na Roho Mtakatifu
katika kupitisha yale haswa Roho wa
Mungu alitaka tuyashike.Sitakuwa na mengi bali nitaeka msisitizo kidogo tuu
kabla ya kuhitimisha semina yetu iliyokuwa na kichwa kisemacho;#JINSI YA KUSHINDA
MAJARIBU KIMWILI NA KIROHO#Nilibahatika kusoma yote waliyo funza wahudumu na
pia changizi mbali mbali na niliguswa sana.Nilipata kuguswa na njia hizi mbili;
1-Kushika
Neno kwa ufahama,kulitafakari kwa undani zaidi na kuliishi kama linavoelekeza.
2-Kujikita
katika kulitenda Neno katika maisha yetu kimwili,yani kulifanyia kazi ya Mungu.
~Baada
ya Yesu Kristo kuwaita watu na kuanza kuwahubiria katika Galilaya,aliwaita
wavuvi hawa,Simon na ndugu yake,Andrea,kisha
akawaita Yakobo na ndugu yake,Yohana.Yesu Kristo aliwaita hawa watu ili kuwa
wanafunzi wake, ambapo walitakiwa kujifunza vyema Neno kisha waje kupewa kazi
kama mitume.Ndugu zangu katika Kristo imekuwa mara nyingi sana tunaposoma
vitabu vya watumishi mbali mbali hatuangalii maneno yenye utashi wa kiroho na
ukimbilia yale yenye utashi wa kimwili,Wanadamu leo tunasema tunamtegemea
Mungu,tunasema tunamtanguliza Mungu ila siyo kivitendo bali tunayosema yote
yanaishia hewani ,hewani kivipi!yanii kimaneno na siyo kivitendo.Nasema hivi
kwa maaana kwamba Yesu Kristo ndiye aliyewachagua watu wale;siyo wao
waliojichagua wala siyo wao waliojichagulia kazi ile.Leo kila mmoja wetu anapo
mahali pa kufanyia huduma lakini siyo wote waliokuwa radhi kumfuata Yesu kristo
ili kumruhusu yeye kutuongoza na kuwa ndiye mwenye kutuchagulia sisi;
![]() |
Mr. & Mrs. Nelson |
-Kazi.
-Biashara.
-Vipawa.
-Ndoa#mke/mume
-Katika
kulitekeleza hili yani ukaitwa kama akina Simon na ndugu yake,Andrea ,kisha Yakobo
na ndugu yake, Yohana ,fahamu kabisa utaitajika kupimwa kwa kupewa JARIBU; na
jaribu hilo litakuwa la kiMungu kama alivosema Katibu Mkuu katika Neno alilo
tuhubiria na utapewa Jaribu ambalo ukilishinda basi litakupa uhalali wa wewe
kuwa;
-Muhudumu
wa Kweli utakaye tumiwa vyema na Roho Mtakatifu ukihudumu katika Injili ya
kweli ile ya Kristo.
-Kazi
ya kweli itakayo kupatia muda wa kumtukuza nayo Mungu,itakupa kipato,itakupa maendeleo
na itakuongeza utumishi wako katika Ufalme wa mbinguni.
-Biashara
ya kweli kimwili na kiroho,yenye faida za kuonekana zenye kumrudishia Mungu
shukrani.
-Vipawa
sahihi vyenye ushuhuda wa kweli wa kumvua Mwanadamu yule asiye amini Ukuu wa
Mungu katika Utatu Mtakatifu.
-Ndoa
yenye Amani,Faraja na Upendo ule wa tunda la roho ulionenwa katika Kitabu cha Wakorintho
na kujidhihirisha kwa Yesu Kristo pale msalabani.
-Kwenye
maisha ya sasa tumekuwa tukiishi kama
wanadamu wenye shingo ngumu sana,mara nyingi utakuta tunaenda makanisani kama
waumini lakini hatuoni ongezeko la imani zetu na hata tukitaka kuongezwa
tunashindwa tukifika kiwango au tunaanguka kwenye Interview/Mtihani ambao
tunajifunza hapa kama JARIBU,na kuishia kulalamika.Tunapokuwa chuo au tunapofanya
biashara flani,ama kazi yo yote,na ukagundua vitu hivi haviongezeki chukuwa hatua.Utaona ukianza vina ishia nusu,ukienda
ukafika haviendelei vinakufa,utavianda na vitaonyesha mwanga mara giza.hatua
hapa ni kurudi darasani ukajifunze kushinda MAJARIBU mbayo ndiyo MTAJI wa
MAFANIKIO yako.Njia zimetasha tajwa sana.KUSHIKA NENO NA KULISHI/KUOMBA BILA
KUKOMA.
-Biblia
inatufunza juu ya haya kwenye habari ya kipindi cha Yesu Kristo,katika sinagogi
moja ambalo Yesu kristo alikuwepo kumbe alikuwepo na kijana ambaye alikuwa
amepagawa na pepo mchafu.Jambo la kushangaza ni kwamba Yesu Kristo hakukemea
bali huyu pepo ndani ya huyo mtu akaanza kupiga kelele kwamba Yesu Kristo
amuachie alivyo ndani ya maisha ya huyu Kijana.Pepo hili lilifanya hivyo maana
lilishazoea kuishi na huyu Kijana na mbaya zaidi Biblia inatuambia huyu kijana
alikuwa mshirika wa siku nyingi wa hilo sinagogi na bado ibada hizo za sinagogi
hazikuweza muweka huru.
-Sikia
mtu wa Mungu unaye soma hitimisho hili nikuhubirie,tizama umekuwa mkristo siku
nyingi na una pepo;(pepo la tabia chafu kadha wa kadha zilizoonywa katika
Torati,tizama uwovu wa aina nyingi uliotajwa kama kitu cha kuepukwa bado
umekushika mfano wa pepo,shida na taabu za kutosha ulizopitia na unazopitia
zimekaa kama pepo na kuridhika,umaskini kimwili na kiroho umekukaa kama pepo,hofu
kiimani na kimtizamo imekaa nawe bila mabadiliko kama pepo,macho ya rohoni
yasiyo na uwezo mzuri wa kumuona mumeo au mkeo,ubongo wa rohoni usio na ufahamu
wa kutosha wa kutambua Baraka za Bwana,roho za visasi,vinyongo),haya kwenye
mabano ni baadhi ya mifano inayofananishwa na yule pepo iliye kuwa ndani ya kijana,kijana muhumini wa
sinagogi.
~Sikia
mwana wa Mungu leo hapa PLACE OF PEACE COMMUNITY tunakuambia kaa tayari maana
Yesu Kristo yuko hapa kukueka huru,huna haja ya kuangaika,wewe jitahidi kutulia
kwa Mungu,shika unayofunzwa hapa na jitahidi kufanyia kazi na utaona tuu hayo
yaliyofananishwa na pepo wa kijana wa sinagogi yataenda kufunguliwa.Leo kupitia
nguvu ile Yesu Kristo aliyokuwa nayo pale sinagogi,nakuambia hilo pepo halina
HAKI ya kuishi ndani yako,na Yesu kristo leo anakwenda kuviamuru
vikutoke,AMENI.
-Nikuache na ‘’home work’’Je,watu wanasikia habari za
Yesu Kristo kutoka kwetu wakati sisi tunapokwenda ofisini?biasharani?chuoni?mashuleni?mtaani?au
majumbani mwetu pindi tukitoka kwenye sehemu Injili ya Kweli yaani habari za
maisha ya Yesu Kristo,Injili ya kweli ya Ukuu wa jina la Mungu!Injili ya kweli
ya Ahadi za Mungu kwa Wanadamu! Agano la Mungu kwa wanadamu!na mahubiri hayo
unapata,Heman,Semina, au Makanisani?.#Barikiwa
sana Mwana wa Mungu uliye fanikiwa kusoma hadi mwisho na ukatunzwe na neno hili
ukisaidiwa na Roho Mtakatifu kulifanya likawe kweli yani likawe ni sehemu ya
maisha yako(LIFESTYLE).
0 comments :