Nashukuru
kwa semina ya wiki hii ambayo kwa kweli inafunza SANA.Mratibu umegusa kitu
ambacho kinamgusa kila mmoja wetu kwa aina yake, "Jinsi ya kushinda
majaribu kiroho na kimwili"
MAJARIBU NI NINI?
Hili
NENO lina definition nyingi lakini inalenga zaidi ushawishi KUTENDA KINYUME NA
MAPENZI YA MUNGU. Kuna aina nyingi za majaribu lakini niyaongelea majaribu ya
aina mbili
1 MUNGU
MWENYEWE
Mwenyezi Mungu
huwa ana tujaribu , lakini Mwenyezi Mungu hatujaribu sisi kwa ajili ya
kutuumiza au kutukomoa, Mwenyezi Mungu anatujaribu ili KUTUPIMA IMANI YETU KWAKE, na ukiangalia wale wanaopata majaribu makubwa ni wale watu wenye imani kubwa kwa Mungu, Mungu hujaribu
watu wenye haki ( ZABURI 11:5 ), angalia wengi waliojaribiwa hata
zama zile, kina Ibrahim, Ayubu na hata YESU KRISTO mwenyewe.
![]() |
Brother Johnson Mshana Katibu Mkuu pPc |
2 JARIBU
LA SHETANI
HILI LIKO TOFAUTI NA LA MUNGU, JARIBU la shetani ni kumjaribu mtu mwenye imani
kujaribu kumpotosha kwa kumpa ahadi nzuri nzuri, lakini pia HUJARIBU wale wenye imani Haba kwa
kuwapa anasa na kupenyeza usahaulifu wa kumuabudu Mungu, naamini itakuwa
umeelewa tofauti kati ya JARIBU la
kimungu na la kishetani.
Wapendwa
katika bwana, tumekuwa tukipata majaribu SANA katika maisha yetu haya, na
majaribu hayajaanza jana wala Leo, ni toka enzi na enzi kama ukisoma biblia
utaona manabii wengi tu hata watu wa kawaida wa kipindi kile
walivyojaribiwa.Hata Leo tunakutana na majaribu
na mitihani midogo kwa mikubwa, wengi wanashindwa KUKABILIANA nayo ndio maana unasikia watu wanajitoa hata UHAI wao wenyewe kwa kushindwa kuhimili
mitihani au majaribu ya maisha.
TUNAJARIBIWA ili KUPIMWA UIMARA WA IMANI YETU KWA MUNGU,
lakini pia tunajaribiwa ili KUMTAMBUA
MWENYEZI MUNGU (Daniel 2:28-29 , 1 Petro
1-12 ).Tumekuwa tukiishi maisha ya
kidunia na kumsahau Mungu, Mwenyezi Mungu pia ANATU-MISS, so ili atuvute kwake anatupatia ka JARIBU kadogo na ikifikia mahali huoni msaada wowote LAZIMA UKIMBILIE KWA MUNGU, angalia
Mungu wetu alivyo mwema, yaani hata uwe ume mfanya nini, ukimrudia anakupokea
kwa mikono miwili.Kama watoto wa Mungu, Kama wapenda KRISTO basi hatuna budi kufanya haya yafuatayo ili kushinda haya
majaribu au mitihani ya maisha inayokuja mbele yetu
1. KUAMINI.....ukishaamini kwamba kuna Mungu, anayejua
kila kitu KUHUSU wewe, kwamba NDIYE anayekulinda, toka uko tumboni
kwa mama YAKO NDIYE anayefuatilia
kila kitu chako BASI UTAWEZA PIA KUAMINI
KWAMBA HATA LIJE TATIZO GANI BASI ATAKUVUSHA.
2. KUJIAMINI..........ni lazima pia ujiamini mwenyewe ,
unaweza ukawa kabisa unaamini kwamba Mungu yupo lakini kutokana na KUTOJIAMINI kwako ikakupa woga wa
kufanya Yale unatakiwa kufanya ambalo lita kuweka karibu zaidi na Mungu.
3. KUTAFUTA MAARIFA........wote hapa tumesoma, japo hatulingani
elimu, kuna ile unakuta unakabiliwa na MTIHANI labda wa kumaliza kidato cha nne
au cha 6, huwa tulikuwa tunachukua PAST
PAPERS, mitihani iliyopita ili kutafuta mbinu mbalimbali za ufanyaji MASWALI katika kuukabili MTIHANI utakaokuja mbele, naamini hii
kila mtu kafanya.Sasa hata kwenye maisha ya kiroho haya TUNAISHI, tunatakiwa kutafuta maarifa kwa KUSOMA BIBLIA, ukisoma biblia utajua na utakuwa na mbinu za kujua
kukabiliana na matatizo au majaribu.Wapendwa,
tumekuwa wavivu SANA wa kusoma na ndio maana TUNAPIGWA SANA NA MITIHANI na tunashindwa ku-fight back sababu HATUNA MBINU, Mungu wetu aliye mwema SANA ametuwekea kila kitu wazi ni ile
tu kwamba tumekuwa wavivu, tu jiweke katika kusoma biblia ili kujua mbinu za KUKABILIANA na MAJARIBU.
Basi
Mungu wetu aliye mwema azidi kutuongoza katika roho na kweli kuweza kuyashinda
majaribu
MBARIKIWE
SANA
0 comments :