Somo la Leo 09/09/2015

Shaloom  Wana wa Mungu. Nawasalimu nyote Katika Jina la Yesu

Namshukuru Mungu kwa asubuhi njema ni matarajio yangu ninyi nyote mmeamshwa vyema katika uzima wake.Basi ni wasaa mwengine mzuri wa siku hii ya Jumanne tukiendelea na semina yetu yenye kichwa kisemacho#Jinsi ya kushinda majaribu kiroho/Kimwili kama Mwanadamu#.Kaka Mugabe jana alifungua semina yetu na alitueleza msingi wa haswa wa wapi Jaribu linatoka na akatupa namna mojawapo ya kushinda akisema kwa habari ya kushika Neno la Mungu,jioni Dada Irene akaeka msingi nay eye akamtumia  Ayubu na kutoa tahadhari kwamba sio lazima Jaribu litoke kwa Mtu mbaya bali ata mtu wa karibu sana nawe ataweza kufanyika Jaribu.
Na Mr. Nelson...Mratibu
~Leo nataka tukatizame upande mwengine wa Jaribu na kabla sijaingia kwenye Neno ntapenda nirudi kwenye neno la jana toka kwa Kaka Mugabe,kuhusu kipindi Yesu Kristo anajaribiwa na Shetani.Shetani ni mjanja sana na mwenye mbinu nyingi.Kwanza kabisa yeye alijaribu kumwambia Yesu Kristo kwamba Bwana alikuwa na kila haki ya kuyageuza mawe kuwa mkate kwa sababu Yesu Kristo kweli alikuwa Mwana wa Mungu.Maneno yale"Ukiwa ni Mwana wa Mungu,"hayana maana ya kwamba Shetani alikuwa na mashaka na Yesu Kristo kwamba hakuwa Mwana wa Mungu.Maneno haya kweli  yanamaanisha kwamba‘Kwa vile wewe ni Mwana wa Mungu,’au "Kwa sababu wewe ni Mwana wa Mungu".Jaribu hapa lilikuwa wapi?Lilikuwa katika Shetani kujaribu kumfanya Yesu Kristo kuyageuza mawe yale kuwa mkate kwa ajili ya faida yake tu,ili kujipendeza mwenyewe.
~Tuingie kwenye Neno letu la leo na tukasome  kitabu cha,#Wamuzi 7:4 BWANA akamwambia Gideoni; Hata sasa watu hawa ni wengi mno; uwalete chini majini, nami nitawajaribu huko kwa ajili yako; kisha itakuwa ya kwamba yule nitakayekuambia, Huyu atakwenda pamoja nawe, ndiye atakayekwenda pamoja nawe; na mtu yule nitakayekuambia, Huyu hatakwenda pamoja nawe, basi mtu huyo hatakwenda.
~Kama nilivoanza na utangulizi tunagundua Shetan ametumia majaribu kwa faida yake na majaribu yakawa faida ya Kristo pia.Hapa tunasoma habari za Gideoni ambaye alikuwa mtumishi mzuri sana wa Mungu tena yule aliyekuwa akiitisha mahitaji kwa maombi ya vitendo.Mara nyingi sana kama wanadamu tumekuwa tukisikia watu wakichukulia Majaribu kama Mikosi,Laana,shida za dunia au dhambi flani.Bila kusahau majaribu yana pande mbili:
1-Upande wa Mungu kama kipimo cha mcha Mungu na Imani yenye utayari.
2-Upande wa shetani kama njia ya kukupotesha usahihi wa kufikia Mbaraka wako na kuangukia kwenye Uovu.
~Ukisoma Biblia utafahamu Gideoni aliteuliwa na Mungu, akiwa ni mtoto mdogo wa Yoashi. Mungu akamteuwa ili kwenda kuwaokoa wana wa Israel uko MIDIANI.Na ndipo alipomuitisha Mungu mambo kadha kupata uwakika wa yale anataka kufahamu toka kwa Mungu.Katika Neno hili mwana wa Mungu tunasoma Gideoni anapewa ahadi na Mungu katika kupatiwa watu sahihi ,hii ilimaanisha Gideoni hakuwa ametambua vyema kwa kiasi cha  uwezo wa hekima watu sahihi wa kuongozana nae katika ukombozi na ndio maana  akaitaji uwakika kwa Mungu.Hii ata leo ipo hapa duniani,sisi kama wanadamu bado hatuna uwakika wa kumsemea mtu kama mtu kamili ila Mungu kwa uwezo wake na kwakuwa yeye ndio muumbaji wetu basi atakuwa ndio 100% kutupa uwakika wa mwanadamu sahihi kwa jambo sahihi.
~Ndugu zangu wana pP,neno hapa linazungumzia Jaribu toka kwa Mungu ili kutoa jibu sahihi na kupata watu sahihi,Jaribu la Mungu katika Neno hili linaweza kuja kwako leo na hata sisi hapa Katika Jumuiya ya Mahali pa Amani (pPc)na ata kwako msomaji katika wengi flani mliyojikusanya ili kufanya huduma litakuja.Tuko wengi hapa na tunaonyesha ule uhitaji wa kutii kiu ya kumjua Mungu na kutumiwa kama Ishara au Alama za mambo yake na Wana wa Ufalme wake,bali lazima tuta pimwa kwa kujaribiwa,sijajua jaribu litakuwaje ila lazima tutapimwa na wale tutakuwa tumepita basi hao ndio haswa tutaendelea na Jumuiya.Sikutishi ila nakuekea msingi kwa maana Mungu wetu anafahamu uhitaji wa Huduma yake na anafahamu fika  nani na nani wanaitaji kufanywa sehemu ya huduma zake na wangapi wako tayari kuona Mungu anatokea katika maisha yao, hivyo  tujitahidi sana kujifunza kwani kunafaida kubwa na nzuri ukihakikiwa na Mungu kumtumikia.Basi kwa sasa nikuache na Tafakari hii na Roho wa Mungu atuguse tutaenda kujifunza zaidi kupitia neno hili juu ya sisi kuitisha  jaribu katika kupata uwakika kwa Mungu.Barikiwa sana.

3 comments :