Neno la leo 16/09/2015

Shaloom wana wa Mungu

Awali ya yote naomba kusema kwamba ntammiss Brother George na nikuombe MpP usiache kumuombea ili Roho Mtakatifu akampe usaidizi wa kukamilisha hiyo Task arudi Hema akija kumshuhudia.Baada ya kusema hayo na kumuamini Mungu atasikia hilo basi tuende kujifunza Neno la Mungu kupitia kichwa kisemacho#Unahitaji kuomba hadi upoke ombi lako#.Ratiba leo inaonyesha MySoulMate angewalisha ila kuna jambo limetokea basi neema ya Bwana iwe nanyi kupitia mimi muda huu.Kuna kipindi cha utoto ilikuwa kuna muda unacheza na watoto wenzako na ghafla mwenzio anakuja na kitu na badala ya kumuomba "directly ",unapitia vitu visivo kuwa na mwelekeo wa kumuomba,utaruka sarakasi,unacheza ngoma,utatoa vichekesho,utataka kumbeba basi tuu ukihisi atafurahii na kukupa alichobeba..Ghafla anakuja mwengine na kusema"Teddy naomba ngumbiti".anampatia na inaisha.unabakia ukitoa.
Fungua tena biblia yako iwe kwa simu au uko nayo..tukasome Neno la tarehe ya leo alilotupa Mrs Jane akilileta kwa Kiingereza ila sisi tutaenda kulisoma kwa kiswahili..imeandikwa ~Marko10:38 Yesu akawaambia, Hamjui mnaloliomba. Mwaweza kunywea kikombe ninyweacho mimi, au kubatizwa ubatizo nibatizwao mimi??
~Tuombe~
 Baba yetu uliye mbinguni,tunasema asante kwa kutupa muda huu wa kujifunza,shika akili zetu,roho zetu na muda wetu,kwa pamoja vikasaidiwe na Roho Mtakatifu ili kusoma na kuelewa neno lako kiusahihi,kwa ufalme ni wako,na nguvu,na utukufu,pasipo mwisho.
 Amen!!
Mr. Nelson Njau, Ath


~Neno linasema Yesu Kristo akawaambia,unapoona kwenye biblia kuna alama hii(,).inakupa kupumzika kisha utafakari,ujijengee picha ya kusikiliza na wewe..."Hamjui mnaloliomba".kwa hali ya kawaida tuu mwana wa Mungu maneno haya ya Yesu yanakupa picha kwa kuna kilichofanyika na ndio akagundua hawajuii...Neno "Hamjui".haliwezi kuwepo mahali kama hakuna"unajua".yani lazima haujui iwe na unajua.Kwahiyo hapa Yesu Kristo alishawaona hao wanadamu aliokuwa anawaambia ila sasa leo unasoma wewe hivyo unaposoma ukakutana na alama ya (  ,  )inakupa nafasi ya kujieka wewe,akawambia,utaanza kuwaza vile ulikuwa unaomba,vile haupokei ombi,vile hauombi hadi ukapokea ombi lako,nini kinakwamisha,nini kinafanya sipatagi,je nayo pata ni matokeo sahihi ya nilicho omba!!!.Sio siri kama mfano nilio ananza nao ni kwamba wanadamu leo tumekuwa kama watoto wa aina mbili nilioanza nao kama mfano,utaona mtoto wa kwanza ndio wanadamu wengi wa leo tulivo,utumia muda mwingi kufanya vitu ili Mungu avione kisha atupe,utakimbilia ishara,utakimbilia kutoa,utakimbilia kufanya baridi na moto usieleweke.Utambeba Yesu ukiwa "fake".ukidhani atakupa hitaji lako,Kisha atakuja mtoto wa pili ambaye anajiamini.Anajiamini kuwa hana cha kumkosesha kupokea na aliamini ataomba na atapewa atapewa kwakuomba kwa kweli toka moyon mwake,ata omba kwa tamaa bali kwa kuwa ana hitaji.Basi utaitaji kujianda mbele za Mungu mpendwa kabla ya kwenda,wengi hawana uwakika kuwa Mungu anauwezo na ukiombacho.Hivyo mtoto wa pili alifahamu alichobeba mwenzie anauwezo nacho kumpatia.Neno linaendelea hapa likisema.."Mwaweza kunywea kikombe ninyweacho mimi".au kubatizwa ubatizo nibatizwao mimi??..tutaendelea baadae kidogo.Barikiwa sana mpendwa.Ukatafakri zaidi.

0 comments :